Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
No Thumbnail Available
Date
2023-03-06
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
East African Journal of Swahili Studies
Abstract
Utafiti huu ulichunguza matumizi ya Kiswahili katika mawasiliano na uongozi
wa kidini katika shule ya
wasichana ya Itigo. Ulilenga kubaini jinsi lugha ya
Kiswahili hutumika katika kuwasilisha maudhui ya kidini, sera za matumizi ya
lugha, na athari ya matumizi ya lugha ya Kiswahili katika kuwasilisha ujumbe wa
kidini. Nadharia ya umilisi mawasiliano yake De
ll Hymes (1966) iliongoza
utafiti. Data ilikusanywa kwa kutumia hojaji, mahojiano na uchunzaji. Wanafunzi
thelathini wa kidato cha nne, viongozi kumi wa kidini wa wanafunzi na kasisi
mmoja wa shule walihusishwa katika ukusanyaji wa data. Matokeo yalibaini
kuwa sera ya lugha katika shule ya wasichana ya Itigo ilipendelea matumizi ya
Kingereza kama lugha ya mawasiliano. Wanafunzi walisema kuwa lugha ya
Kiswahili inapotumika katika mahubiri, ujumbe hueleweka zaidi. Vilevile,
ilidhihirika kuwa viongozi wa kidin
i wa wanafunzi hutumia lugha ya Kiswahili
kuwasiliana katika mikutano yao lakini wao huandika kumbukumbu kwa lugha
ya Kiingereza. Isitoshe, ilibainika kuwa lugha anayoitumia zaidi kasisi wa shule
katika mahubiri yake ni Kiingereza. Licha ya uwezo wa Kiswah
ili katika
kufanikisha mawasiliano kuhusu maswala ya kidini shuleni, Kiingereza ndicho
hutumika zaidi. Kunahitajika mabadiliko katika sera ya lugha shuleni ili kuipa
lugha ya Kiswahili nafasi zaidi katika mawasiliano ya kidini
.
Description
Journal Article
Keywords
Mawasiliano, Dini, Kiswahili, Uongozi
Citation
Melly , J . K ., & Mohochi , E. S . (2023). Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo East African Journal of Swahili Studies , 6 (1), 339 - 3 49 . https://doi.org/10.37284/jammk.6.1.1 42 2
