Kibuspace
Kibuspace is the institutional repository of Kibabii University, the repository preserves the University's research legacy and all aspects of knowledge generated by KIBU community for posterity

Communities in DSpace
Select a community to browse its collections.
Recent Submissions
Matumizi ya Kiswahili katika Mawasiliano na Uongozi wa Kidini katika Shule za Upili Nchini Kenya: Mfano wa Shule ya Wasichana ya Itigo
(East African Journal of Swahili Studies, 2023-03-06) Kipchirchir, Joachim Melly; Mohochi, Ernest Sangai
Utafiti huu ulichunguza matumizi ya Kiswahili katika mawasiliano na uongozi
wa kidini katika shule ya
wasichana ya Itigo. Ulilenga kubaini jinsi lugha ya
Kiswahili hutumika katika kuwasilisha maudhui ya kidini, sera za matumizi ya
lugha, na athari ya matumizi ya lugha ya Kiswahili katika kuwasilisha ujumbe wa
kidini. Nadharia ya umilisi mawasiliano yake De
ll Hymes (1966) iliongoza
utafiti. Data ilikusanywa kwa kutumia hojaji, mahojiano na uchunzaji. Wanafunzi
thelathini wa kidato cha nne, viongozi kumi wa kidini wa wanafunzi na kasisi
mmoja wa shule walihusishwa katika ukusanyaji wa data. Matokeo yalibaini
kuwa sera ya lugha katika shule ya wasichana ya Itigo ilipendelea matumizi ya
Kingereza kama lugha ya mawasiliano. Wanafunzi walisema kuwa lugha ya
Kiswahili inapotumika katika mahubiri, ujumbe hueleweka zaidi. Vilevile,
ilidhihirika kuwa viongozi wa kidin
i wa wanafunzi hutumia lugha ya Kiswahili
kuwasiliana katika mikutano yao lakini wao huandika kumbukumbu kwa lugha
ya Kiingereza. Isitoshe, ilibainika kuwa lugha anayoitumia zaidi kasisi wa shule
katika mahubiri yake ni Kiingereza. Licha ya uwezo wa Kiswah
ili katika
kufanikisha mawasiliano kuhusu maswala ya kidini shuleni, Kiingereza ndicho
hutumika zaidi. Kunahitajika mabadiliko katika sera ya lugha shuleni ili kuipa
lugha ya Kiswahili nafasi zaidi katika mawasiliano ya kidini
.
Maadhimisho ya Siku kuu ya Kiswahili Duniani: Upi mwelekeo mwafaka?
(Jarida la Kiswahili Sanifu, 2024-11-27) Miruka, Frida; Mohochi, Ernest Sangai; Ngugi, Pamela; Jagero, Juliet
Lugha ya Kiswahili ni mojawapo ya lugha za Kiafrika zinazozungumzwa zaidi ulimwenguni
ikiwa na zaidi ya wasemaji Millioni 250. Hali hii pamoja na hadhi na dhima ya Kiswahili
katika jamii mbalimbali ilipelekea shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na
Utamaduni (UNESCO) katika kikao chake cha 41 kutangaza Julai tarehe 7 kuwa siku kuu
ya Kiswahili duniani. Hatua hii ilikifanya Kiswahili kuwa lugha ya kwanza ya Kiafrika
kutambuliwa na Umoja wa Mataifa na kuwa na siku maalum ya kuadhimishwa. Katika
maadhimisho ya tatu yaliyofanyika mwaka 2024 kote duniani, Jumuia ya Afrika mashariki
kupitia Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki (KAKAMA) iliandaa sherehe nchini Kenya
kwa kushirikiana na Wizara ya Jinsia, Utamaduni, Sanaa na Turathi. Wadau waliohusishwa
walikuwa baadhi ya wanataaluma, wapenzi wa lugha ya Kiswahili na Jamii ya Waswahili
mjini Mombasa. Maadhimisho haya hata hivyo hayakuwahusisha wadau wote ambao
wamechangia kuiinua lugha hii na kuipa sura ya Lugha ya Ulimwengu. Baadhi yao ni
wataalamu kutoka vyuo vikuu mbalimbali, waandishi wa vitabu, wanahabari na walimu
wa Kiswahili. Mipango ya kuandaa sherehe katika baadhi ya vyuo maalumu haikufua dafu
huku vyuo vingine vikiadhimisha siku hii kando na sherehe iliyoandaliwa na KAKAMA.
Kukifungia Kiswahili katika jamii na utamaduni wa Waswahili pia kunaishusha hadhi lugha
hii kama lugha ya Ulimwengu. Swali linalozuka ni Je, pana haja ya kuweka mpango
mwafaka wa kuadhimisha siku hii? Makala hii inaangazia nafasi ya Kiswahili katika jamii
na kutathmini Maadhimisho ya Siku ya Kiswahili kwa lengo la kupendekeza mikakati ya
kuyaimarisha ili kujenga taswira ya lugha ya Kiswahili kama lugha ya ulimwengu.
Pendekezo kuu la Makala hii ni kuhimiza ushirikiano wa wadau wote katika maadhimisho
ya Siku kuu ya Kiswahili duniani.
Mabadiliko ya Itikadi za Ujinaishaji katika Jamii ya Wakuria
(Jarida la Kiswahili Sanifu, 2024-11-27) Mwikali, Roseline; Mohochi, Ernest Sangai; Ogola, James
Dunia ya leo ya kiutandawazi inawezesha mtagusano wa umma wa kimataifa kidijitali unaoendelea kushuhudia utamaduni chipukizi wa ujinaishaji unaozidi kushika kasi. Hivyo, makala hii inachanganua mabadiliko katika ruwaza za ujinaishaji yanayotokana na athariya elimu ya magharibi, dini, teknolojia, na utawala katika jamii ya Wakuria pamoja na athari zake. Wakuria ni jamii ndogo ya kundi la Wabantu wa Magharibi inayopatikana katika Kaunti ya Migori nchini Kenya kwenye ujirani na nchi ya Tanzania. Ujinaishaji ni sehemu muhimu ya maisha ya jamii ya Wakuria kwani ni utambulisho wao. Aidha, sawa na jamii nyingine zile, ujinaishaji huwa dafina ya historia yao. Nadharia ya Uchanganuzi Hakiki wa Usemi mtazamo wa Kihistoria yao Wodak na Reisgil(2001)ilikuwadira katika uchanganuzi wa data zilizokusanywa. Data ambayo imetumika katika makala hii ilikusanywa kwa njia ya mahojiano ya ana kwa ana pamoja na majadiliano ya makundi. Idadi ya sampuli ilikuwa watu 42; wa kike 18 na wa kiume 24. Makala hii imebainisha kuwa mabadiliko ya kielimu, kiuchumi, kiteknolojia, kiutawala na kidini yamekuwa na athari kubwa kiitikadi katika ujinaishaji miongoni mwa Wakuria. Majilio ya elimu ya magharibi, uhuru wa kufanya biashara, mifumo ya kisiasa na mtagusano wa kiteknolojia umepelekea ukopaji wa majina kutoka makabila mengine nchini Kenya na ulimwenguni kote miongoni mwa jamii ya Wakuria. Hili linamaanisha kuwa itikadi za ujinsia zilizohodhiwa na kushamirishwa na majina ya kiasili ya Wakuria zinazidi kufifia kila uchao.
Matumizi ya Lugha ya Kinandi katika Kuendeleza Kilimo kupitia Vipindi vya Runinga ya Kass
(East African Journal of Swahili Studies, 2025-05-07) Kipchirchir, Joachim Melly; Wamalwa, Eric Walela; Mohochi, Ernest Sangai
Wakulima wengi nchini Kenya hupatikana katika maeneo ya mashambani
ambako mawasiliano mengi huwa katika lugha za kiasili. Vyombo vya habari
ni miongoni mwa asasi ambazo zimechangia pakubwa katika kukuza matumizi
ya lugha za kiasili na kuwahamasisha wananch
i kuhusu kilimo. Kwa sababu
hiyo, juhudi nyingi zimeelekezwa katika kuwafikia wakulima ambao ni
wahusika wakuu katika sekta ya kilimo ili kuwapa elimu ya kujiendeleza.
Lugha ya Kinandi ni mojawapo ya lugha za kiasili ambayo hutumiwa katika
runinga ya Kass.
Utafiti huu ulilenga kuchunguza jinsi lugha ya Kinandi
hutumika kuinua viwango vya kilimo miongoni mwa wanajamii kupitia vipindi
vya runinga ya Kass. Utafiti huu ulifanyika katika kaunti ya Nandi. Uliongozwa
na Nadharia ya Uanzilishi wa Ajenda ya McCombs
na Shaw (1993).
Watazamaji waliteuliwa kinasibu ili kuhusishwa katika utafiti. Watazamaji 264
walihusishwa katika ukusanyaji wa data. Mbinu za hojaji, uchunzaji na
mahojiano zilitumika katika kukusanya data. Vifaa vilivyotumika kukusanya
data ni: mwongozo
wa utazamaji, hojaji na mwongozo wa maswali ya
mahojiano. Data iliyokusanywa ilichanganuliwa kimaelezo kwa kuzingatia
lengo la utafiti kisha ikawasilishwa kwa kutumia asilimia na majedwali.
Matokeo ya utafiti yalithibitisha kuwa lugha ya kinandi inayotumik
a
kuwasilisha vipindi vya kilimo iliwasaidia sana wakulima kuimarisha mapato
katika kilimo. Utafiti huu unatarajiwa kuwa wa manufaa kwa wanajamii kwa
kuwa ulitoa mwanga kuhusu umuhimu wa matumizi ya lugha za kiasili katika
kuinua viwango vya kilimo
Mandhari katika Nyimbo za Kizazi Kipya Mtandaoni Zinazohusu Mapambano Dhidi ya Dawa za Kulevya
(East African Journal of Swahili Studies, 2025-05-12) Ndinyo, Stephen Muyundo; Mohochi, Ernest Sangai; Musungu, Joseph Juma
Mapambano dhidi ya dawa za kulevya ni miongoni mwa masuala
yanayosawiriwa katika nyimbo za kizazi kipya mtandaoni. Katika kufanya
hivyo, nyimbo hizo hutumia vipengele mbalimbali vya kisanii. Mojawapo kati
ya vipengele hivyo ni mandhari, huku usukaji mzuri
wa mandhari ukichangia
fanaka katika uwasilishaji wa ujumbe wa nyimbo hizo. Makala haya
yalichunguza mandhari katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya kupitia
nyimbo za kizazi kipya mtandaoni. Makala yaliongozwa na Nadharia ya
Utendaji katika Fasihi Simul
izi iliyoasisiwa na Wallace Bacon katika mwaka
wa 1957. Muundo wa kithamano mkabala wa kiutendaji ulitumika katika
makala haya. Uchanganuzi wa yaliyomo ulitumika kukusanya data kutoka kwa
video za nyimbo za kizazi kipya kuhusu dawa za kulevya katika mtanda
o wa
YouTube ambao uliteuliwa kimaksudi. Aidha, nyimbo ziliteuliwa kimaksudi.
Kisha, nyimbo hizo zilitabakishwa kidhima na kwa kurejelea aina tofauti za
dawa za kulevya zinazosawiriwa. Jumla ya nyimbo 5 zilitumika. Data
iliwasilishwa kwa kutumia maelezo ya
kifafanuzi na mijadala, mifano na
dondoo kutoka kwenye uchanganuzi wa yaliyomo. Matokeo yalionyesha
kwamba aina mbalimbali ya mandhari yalibainika katika video za nyimbo za
kizazi kipya kuhusu mapambano dhidi ya dawa za kulevya mtandaoni.
Mandhari ya klab
u, nyumbani, barabarani, mjini, mtaani na yale ya wakati
yalitumika katika vita dhidi ya uraibu wa dawa za kulevya katika jamii. Aina
hizi za mandhari zilotoa mchango katika kuwasilisha ujumbe kuhusu vita dhidi
ya dawa za kulevya. Utafiti unapendekeza kwam
ba kuna haja ya kuchunguza
mandhari kuhusiana na mapambano dhidi ya dawa za kulevya kwa kurejelea
aina nyinginezo za nyimbo mbali na zile za kizazi kipya. Pili, ni vyema
mandhari yatafitiwe katika tanzu nyingine za fasihi pepe kama vile vichekesho,
filamu
na vipindi vya runinga kwa kurejelea suala la dawa za kulevya
.
