Repository logo
Communities & Collections
All of DSpace
  • English
  • العربية
  • বাংলা
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Ελληνικά
  • Español
  • Suomi
  • Français
  • Gàidhlig
  • हिंदी
  • Magyar
  • Italiano
  • Қазақ
  • Latviešu
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Српски
  • Svenska
  • Türkçe
  • Yкраї́нська
  • Tiếng Việt
Log In
New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Simiyu, Fred Wanjala"

Filter results by typing the first few letters
Now showing 1 - 11 of 11
  • Results Per Page
  • Sort Options
  • No Thumbnail Available
    Item
    A Critical Discourse Analysis of Linguistic and Discursive Strategies Used in Kenya’s Citizen Television Advertisements to Display Gender Ideologies
    (East African Journal of Arts and Social Sciences, 2020-10-14) Mayoyo, Edna Magoma; Khaemba, Josephine; Simiyu, Fred Wanjala
    The present study sought to examine how linguistic devices and discursive strategies used in Kenya’s Citizen TV ads which pattern men and women differently according to gender well-being. This thereby results in unconscious rationalisations of social constructions. Using observation as the main tool of data collection, a corpus of fourteen adverts sourced from one mainstream media station, Citizen TV were purposively sampled, observed by the researcher, transcribed into data, coded, then thematically analysed using techniques of content analysis. Guided by Fairclough’s Critical Discourse Analysis theory which provided the framework for analysis, the study adopted a qualitative, case study research design. The research design provided in-depth information about the phenomenon in order to establish the discursive and linguistic strategies used in the TV ads and how they mirror society’s system of values, attitudes and beliefs about men and women. The findings of this study indicated that gender ideologies that affect how meaning is made out of Kenyan TV ads were embedded in linguistic structures, social processes and manoeuvres.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Dhima ya Futuhitandao Katika Kukabiliana na Masuala ya Afya ya Akili Miongoni Mwa Wakenya
    (Eastern Africa Journal of Kiswahili, 2025-06-09) Magambo, Emilly Angushi; Simiyu, Fred Wanjala; Orina, Felix Ayioka
    Fasihi kupitia utambuzi na tanzu zake tofauti tofauti, tangu jadi, imekuwa na majukumu mahususi ya kutekeleza katika jamii. Kama utanzu mojawapo wa fasihi simulizi, futuhi imetumika pakubwa katika vyombo vya habari kama vile televisheni na redioni kuwafurahisha na kuwachekesha watazamaji na wasikilizaji. Hata hivyo, katika siku za hivi karibuni, futuhi imechukua mkondo tofauti katika uwasilishaji wake. Hii ni kwa sababu ya njia mpya ya mawasiliano ya teknolojia ya kisasa ambayo imezua mitandao ya kijamii kama vile Facebook, TikTok, Twitter, Instagram na YouTube. Mbinu mpya za kiteknolojia sasa zipo kwa wingi kuliko wakati mwingine wowote. Licha ya mkurupuko wa mbinu hizi, tusisahau kwamba tangu jadi futuhi imekuwa muhimu katika jamii mbalimbali. Lakini sasa futuhi imekuwa karibu zaidi kwa sababu ya teknolojia ya kisasa. Vile vile, suala la afya ya akili limekuwa nyeti miongoni mwa Wakenya. Hivyo basi, kukawa na haja ya kuchunguza zaidi kuhusu futuhi katika mitandao hii ya kijamii na afya ya akili miongoni mwa Wakenya. Mada hii vile vile ilichaguliwa kwa sababu tafiti ambazo zilihusu futuhi, ziliegemea futuhi katika vitabu vya riwaya na tamthilia na hazikujikita katika suala la afya ya akili. Hivyo basi, makala haya yalinuia kujaza pengo hili kwa kutafitia futuhitandao na afya ya akili miongoni mwa Wakenya, na hasa kwa kuzingatia futuhi zinazopatikana kwenye mitandao ya kijamii hususan Facebook, Twitter na YouTube. Makala haya yalitumia nadharia ya Burudiko ya Sigmund Freud. Utafiti huu ulitumia muundo wa kiethnografia, mkabala wa kithamano. Data kuhusu futuhitandao ilikusanywa kwa mbinu ya Uchanganuzi wa Yaliyomo. Uteuzi wa sampuli ulikuwa wa kimakusudi na kinasibu. Umuhimu wa makala haya ni kuwa, matokeo yake yatasaidia katika ufundishaji wa futuhi. Inapendekezwa kuwa tafiti zaidi zifanywe kuhusu suala la afya ya akili kwa kurejelea vipera vingine vya fasihi simulizi.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Identifying and use of imagery in selected songs of Mrisho Mpoto
    (Research Journal in African Languages, 2021-06-18) Mandila, Geoffrey; Opande, Nilson; Simiyu, Fred Wanjala
    Tasnifu hii inalenga kushughulikia nyimbo teule za Mrisho Mpoto. Imeshughulikia jazanda katika nyimbo hizi kwa kutumia nadharia ya kimtindo. Kazi hii inadhamiria kuchanganua jazanda katika nyimbo za Mpoto na jinsi ambavyo jazanda hizo zinachangia kuwasilisha maudhui katika nyimbo hizo. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya kimtindo ambayo inahusu matumizi ya maneno kisanaa hivyo basi kuifanya lugha kuwa ngumu au rahisi, kuzua hisia za mwandishi zinaonekana, zikionyesha dhihaka, mapenzi, matumaini, ukali au kejeli, matumizi ya tamathali za usemi kama vile tashbihi, sitiari, tashihisi na kadhalika kwa wingi, uteuzi wa msamiati uliotumika huleta mvuto kwa hadhira lengwa, matumizi ya lugha kwa kujikita katika miktadha maalumu katika kusimulia hadithi au kueleza matukio. Hata hivyo, utafiti huu umejikita katika mihimi mitatu mikuu; maneno hutumiwa kisanaa hivyo basi kuifanya lugha kuwa ngumu au rahisi; hisia za mwandishi zinaonekana, zikionyesha dhihaka, mapenzi, matumaini, ukali au kejeli kutokana na matumizi ya lugha; uteuzi wa msamiati uliotumika huleta mvuto kwa hadhira lengwa. Matokeo ya utafiti huu yalibaini kuwa nyimbo za Mrisho Mpoto kutokana na matumizi ya jazanda, wapenzi wake wengi hawazielezi vyema. Hivyo basi tukapendekeza tafiti zaidi kufanywa katika nyimbo hizi katika vipengele vingine vya kisanaa.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Maelezo Kinzani ya Vipengele vya Sarufi ya Kiswahili Katika Vitabu Teule vya Shule za Upili Nchini Kenya
    (East African Journal of Swahili Studies, 2021-06-01) Wanyonyi, Fred Wanjala; Misiko, David Wasike; Simiyu, Fred Wanjala
    Dhamira ya makala hii ilikuwa ni kuonesha tofauti za kimaelezo baina ya waandishi wa sarufi kama inavyojitokeza katika ufundishaji na ujifunzaji wa Sarufi ya Kiswahili katika shule za upili hapa nchini Kenya. Uchunguzi huu uliongozwa na Nadharia ya Sarufi Amilifu na nadharia ya Ujifunzaji Kitajiriba. Sarufi Amilifu ni ya Simon C. Dik (1978). Nadharia hii inashikilia kwamba, uzingatifu wa sarufi ya lugha unadhihirika katika utendaji wa lugha hiyo ambao unakuzwa katika matini inayoandaliwa na wataalamu wake. Nayo nadharia ya Ujifunzaji Kitajiriba iliyoasisiwa na David Allen Kolb mnamo mwaka wa 1984 inaangazia matumizi ya tajiriba katika ufundishaji na ujifunzaji. Kundi lengwa lilikuwa ni waandishi wa Sarufi ya Kiswahili, walimu wa Sarufi ya Kiswahili na wanafunzi wa kidato cha tatu. Tulitumia mbinu za usampulishaji wa kinasibu na usampulishaji wa kimakusudi kuteua sampuli iliyokusudiwa tukizingatia asilimia 30 ya jumla ya idadi lengwa. Walimu 12 na wanafunzi 120 waliteuliwa kushiriki katika uchunguzi huu. Data ilikusanywa kwa kutumia mbinu ya uchanganuzi wa yaliyomo, hojaji na mahojiano. Data katika makala hii iliwasilishwa kupitia maelezo, majedwali na asilimia. Matokeo ya makala hii yalionesha kwamba, waandishi wa Sarufi ya Kiswahili wanakinzana katika ufafanuzi wa baadhi ya vipengele vya Sarufi ya Kiswahili katika shule za upili nchini Kenya. Uchunguzi huu utakuwa wenye umuhimu kwa walimu wa Sarufi ya Kiswahili, wanafunzi, wataalamu wa Sarufi ya Kiswahili na wale wanaoandaa na kuchapisha vitabu vya Sarufi ya Kiswahili kwa kutambua vipengele tata katika Sarufi ya Kiswahili. Makala ilipendekeza Taasisi ya Ukuzaji wa Mitalaa ya Kenya kuvichunguza upya vitabu vya kiada na ziada vya Sarufi ya Kiswahili ambavyo vimeidhinishwa na wao huku vikiwa na tofauti za kimaelezo.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Maudhui katika Nyimbo Teule Kwenye Kipindi cha Rauka
    (East African Journal of Swahili Studies, 2020-07-15) Chepkwony, Joyce; Simiyu, Fred Wanjala; Adero, Margan
    Utafiti huu unahusu maudhui katika nyimbo teule kwenye vyombo vya habari, mfano ni nyimbo katika kipindi cha Rauka katika runinga ya Citizen. Utafiti ulichochewa na haja ya kutaka kuchunguza nafasi ya vyombo vya habari katika kuhuisha fasihi simulizi kupitia utanzu wa nyimbo. Tafiti za awali zilichunguza tanzu nyingine kama mazungumzo na maigizo. Utafiti huu ulidhamiria hususan: Kubainisha vigezo vilivyotumiwa kuteua nyimbo zinazochezwa kwenye kipindi cha Rauka; Kuonyesha maudhui katika nyimbo teule; Kuchunguza mbinu za lugha zilizotumiwa kuwasilisha maudhui za nyimbo zinazoteuliwa na kuchezwa kwenye kipindi cha Rauka. Utafiti huu ulifanywa kwa kuzingatia muundo wa kimfano unaoeleza kuwa mtafiti huteua eneo au kitu maalum ambacho kitashughulikiwa na kuwezesha kupatikana kwa data za utafiti zilizokusudiwa. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Ajenda iliyoasisiwa na McCombs na Shaw mwaka wa 1972. Nadharia ya Ajenda ilitumika kuhakiki uteuzi wa nyimbo wa kipindi kinachopeperushwa na runinga. Uchunguzi ulifanywa katika idhaa ya Citizen kipindi cha Rauka kinachopeperusha nyimbo za dini. Utafiti uliwahusisha waandaaji wawili wa kipindi cha Rauka cha runinga ya Citizen na watazamaji 68 kutoka eneo la Eldoret, Kaunti ya Uasin Gishu, shule za upili ya wasichana ya Hill School. Kwa ujumla, utafiti uliwahusisha watu 70. Watazamaji waliteuliwa kwa kutumia usampulishaji kimaksudi. Vifaa vifuatavyo vilitumiwa kukusanya data: hojaji kwa watazamaji, usaili kwa waandaaji wa kipindi na mwalimu msimamizi wa masuala ya dini na mkuu wa ushauri na nasaha na kinasa sauti kunasia vipindi vilivyoteuliwa kisha vikachanganuliwa. Data ifuatayo ilikusanywa: Nyimbo zilizochezwa kwenye kipindi cha Rauka ziliteuliwa kwa kuzingatia mada ya siku, muda uliotengewa kipindi cha Rauka, hadhira, masuala ibuka, kuwepo na nyimbo zinazowavutia watazamaji; Utafiti umebainisha kuwa nyimbo zinazochezwa katika kipindi cha Rauka zina maudhui ya upendo, shukrani, msamaha, uvumilivu, heshima, wema na msaada. Data iliyokusanywa ilichanganuliwa kwa kuzingatia nadharia ya Ajenda kwa kubainisha maudhui yaliyomo kisha matokeo yakawasilishwa kupitia maelezo ya kifafanuzi na mfano. Matokeo ya utafiti huu yatakuwa mchango kwa tafiti ambazo zimefanywa kuhusu fasihi simulizi na matumizi yake katika vyombo vya habari. Utafiti huu vilevile utakuwa wa manufaa kwa yeyote atakayefanya utafiti kuhusu fasihi simulizi na vyombo vya habari.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Nafasi Ya Fasihi Simulizi Katika Kuwasilisha Ujumbe Kisheria: Mfano wa Uendeshaji Kesi Za Kitamaduni Miongoni Mwa Babukusu
    (Editon Consortium Journal of Kiswahili, 2020-12-10) Wekesa, Winnie Musailo; Simiyu, Fred Wanjala; Opande, Nilson Isaac
    Utafiti uliazimia kubainisha nafasi ya Fasihi Simulizi katika kuwasilisha ujumbe kisheria. Ulionyesha namna vipengele bainifu vya Fasihi Simulizi vinaweza kutumika kuwasilisha ujumbe kisheria. Ulifanya hivyo kwa kuegemea uendeshaji wa kesi kitamaduni miongoni mwa jamii ya Babukusu. Ili kuafikia lengo hili utafiti ulitumia mbinu ya kithamano. Idadi lengwa ya utafiti ilikuwa jumla ya kesi za kitamaduni tulizohudhuria na kuzirekodi. Utafiti ulijumuisha mbinu ya uteuzi wa sampuli kimaksudi. Uteuzi wa sampuli kimaksudi ulitumiwa kuchagua Chifu, naibu wa Chifu, mwenyekiti wa baraza la wazee na makala maalum yaliyoandikwa kuhusu Fasihi Simulizi na Sheria. Nao uteuzi wa sampuli kinasibu ulitumiwa kuteua mabaraza ya wazee na ya Chifu tuliohudhuria. Waaidha, uchunguzi ulihusisha mbinu za uchambuzi wa yaliyomo, usaili na uchunzaji-shiriki. Njia hizi zilitumika kukusanya data nyanjani na maktabani. Matokeo ya utafiti yalichanganuliwa kithamano. Hii ni mbinu ya kuchanganua data ambayo mtafiti anaeleza na kufafanua matokeo ya utafiti wake kimaelezo. Uchunguzi huu vilevile uliongozwa na nadharia ya Mwingilianomatini. Kwa mujibu wa kesi tulizohudhuria, utafiti ulibaini kuwa kuna vipengele vya Fasihi Simulizi ambavyo vinaoana na hali ilivyo katika taaluma ya Sheria wakati wa uendeshaj kesi kitamaduni miongoni mwa jamii ya Babukusu. Kwa hivyo ni muhali kusema kuwa matini za Kifasihi Simulizi huwa zinachota, kunukuu, kugeuza, kuiga kwa namna ya kufumba, kubeza au kurejelea kwa njia moja ama nyingine matini za Kisheria. Hali kadhalika tanzu zenyewe za Fasihi Simulizi zinaingiliana na kuchangiana katika kutimiza mahitaji ya jamii kupitia shughuli mbalimbali.
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    The Role of Language in Facilitating Culture: A Case Study of the Isukha Community, Kakamega County in Kenya
    (KIBU, 2019-09-06) Simiyu, Fred Wanjala; Kibigo, Mary Lukamika; Choge, Susan Chebet
    The study explores the role of language specifically nouns in portraying masculinity in the Isukha culture during the ritual of Shilembe and the indigenous sport of Mayo. Culture is the way of life of a people. A people’s culture is encompassed in their language. Thus, it is not possible to delink the Isukha language from their culture especially through the praise poetry that is chanted by the artists during bullfighting. The Isukha community from Shinyalu Sub County of Kakamega County, Kenya, participates in bullfighting as a ritual known as Shilembe. This ritual involves two bulls fighting on the grave of a male hero who has died but while alive he killed either a wild animal or an enemy of the community. They also participate in bullfighting as an indigenous sport that is referred to as Mayo. However, the study discovered that the two games are not just done as a ritual and an indigenous sport respectively during bullfighting but rather the praise poems that are chanted possess language aspects that portray masculinity. The study used Hegemonic Masculinity and Critical Discourse Analysis to analyse the language used by the artists in the praise poems. The findings of this study will be helpful in understanding African communities like the Isukha, especially when it comes to male chauvinism.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Tamathali Za Semi Zinazosawiri Ubabedume Katika Majigambo Ya Miviga Ya Shilembe Na Mchezasili Wa Mayo Ya Waisukha, Nchini Kenya Kwa Mtazamo Wa Semantiki
    (East African Journal of Swahili Studies, 2019-09-06) Kibigo, Mary Lukamika; Choge, Susan Chebet; Simiyu, Fred Wanjala
    Makala hii imewasilisha baadhi ya matokeo ya utafiti wa Uzamifu uliotafitia ubabedume katika majigambo ya miviga ya Shilembe na mchezasili wa Mayo katika jamii ya Waisukha nchini Kenya kwa mtazamo wa semantiki. Utafiti huu ulihakiki tamathali mbalimbali za semi ambazo ni chuku, jazanda na majazi miongoni mwa nyingine kwa kutumia mtazamo wa kisemantiki ili kudhihirisha namna zinavyosawiri ubabedume katika miviga ya Shilembe na Mchezasili wa Mayo. Utafiti huu ulifanyika katika Kaunti Ndogo ya Shinyalu, Kaunti ya Kakamega, nchini Kenya. Utafiti huu uliongozwa na nadharia mbili, ya kwanza ni nadharia ya Uwezo-Uume iliyoasisiwa na Robert Bly na kuendelezwa na Izugbara. Inahusu mahusiano ya wanaume na wanawake katika jamii. Nadharia ya pili iliyotumiwa ni ile ya Uchanganuzi Makinifu wa Diskosi (UCHAMAWADI). Nadharia hii ina misingi yake katika kazi mbalimbali za wataalam tofauti ulimwenguni. Nadharia mbili zilitumiwa ili kuoanisha taaluma ya Fasihi na Isimu. Utafiti huu ulitumia majigambo kumi na sita kwa kutumia uchunzaji-shiriki, dodoso, unasaji sauti na ujazaji wa hojaji. Matokeo ya utafiti yalionyesha kuwa lugha ya majigambo inayoghaniwa na fanani hubeba tamathali za semi zinazosawiri ubabedume. Hivyo, sherehe hizi zitumiwe kama jukwaa la kuelimisha vizazi vichanga vya jamii hii kuhusu mila na desturi zao. Utafiti huu umeonyesha kuwa Fasihi Simulizi ya Mwafrika ni hai. Utafitiumegundua kuwa, lugha ni kipengele muhimu katika jamii. Hata hivyo, utafiti umetambua kuwa, wakati mwingine lugha hutumiwa vibaya na wanajamii kumtukuza Mwanamume kupita kiasi na kumpa uwezo na mamlaka dhidi ya mwanamke. Isitoshe, ubabedume umejengwa katika mila, itikadi na utamaduni wa jamii husika. Makala hii imeweka wazi baadhi ya matokeo ya utafiti huu.
  • No Thumbnail Available
    Item
    The dynamics of humour in coital imagery: Reflections on Bukusu Embalu and select East African popular music
    (Taylor and Francis Group, 2022-06-09) Simiyu, Fred Wanjala; Orina, Felix
    Beyond procreation and continuity of the human race, sex and sexuality are a long-lasting creative force in literary art, whether oral or written, and beyond. Indeed, there are an unlimited number of artists whose claim to fame and immortality is their treatment of sex and sexuality in their creations. From traditional to contemporary oral art forms, references to physical sex, enunciation of the feelings and emotions underlying sex, and the accompanying innuendos are practically a social fact that is, however, seldom acknowledged. Also rarely acknowledged is the propensity of artistic sexual references to occasion excitement and amusement among hearers. Artists of all ages are wont to deploy sexual images as inspired by their unique contexts and diverse artistic ends, desires, and aspirations. Indeed, the desire to amuse and move to mirth and laughter, even as salient messages are delivered, may be one of the fundamental motivations. In the present chapter, we look at how coital imagery is deployed by artists in two different sexual humour cycles (old and contemporary, respectively) to arouse aesthetic response of amusement and mirth and, in the process, bring to surface any issues of profound social import. We specifically explore the making of sexual humour in traditional Embalu ritual among the Babukusu of western Kenya, on the one hand, and selected contemporary East African popular music, on the other, with the aim of establishing how the two genres relate in both content and form relative to their idiosyncratic contexts.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Usawiri wa Vijana wa Kisasa katika Riwaya ya Dunia yao ya Kiswahili
    (East African Journal of Swahili Studies,, 2024-01-02) Musembi, Naomi Nzilani; Simiyu, Fred Wanjala
    Makala hii itachunguza usawiri wa vijana katika dunia ya sasa inayobadilika kila uchao. Itafanya hivi kupitia uchanganuzi wa riwaya mpya ya Dunia Yao (2006) ya S.A Mohamed. Utafiti unaonyesha kwamba vijana kote duniani sasa wana utamaduni wao ambao watafiti wanaueleza kama ‘ulimwengu huru’ wa vijana ulio na mitindo na njia za maisha ambazo, vijana hufuata ili kujitofautisha na utamaduni wa wazazi wao. Utamaduni wa vijana kwa kiasi kikubwa ni zao la maendeleo katika jamii za ulimwengu. Kadri jamii inavyosonga mbele kimaendeleo, ndivyo ambavyo utamaduni wa vijana unakuzwa, unaimarishwa na kusambazwa miongoni mwa vijana kote duniani. Vijana wamebuni utamaduni wao kama njia moja ya kuasi dhidi ya utamaduni uliotawaliwa na wazee. Wanataka kujihusisha na tabia kama matumizi ya dawa za kulevya, ushoga, uasi wa maadili ya kijamii, Mitindo mipya ya mavazi, muziki miongoni mwa tabia nyingine ambazo wanajua huwatenga wazee. Hii ni tabia ibuka ya vijana kupania kuonyesha nguvu na uwezo wao katika jamii. Ujumbe wanaopitisha ni kuwa hawako tayari kushiriki utamaduni unaowadhibiti na kuwanyima nafasi yao katika jamii. Malengo mahususi yatakayoongoza makala haya ni pamoja na kuangazia sifa za vijana wa kisasa na wakati huo huo kufafanua njia mabazo wanajamii wanaweza kutumia ili kujaribu kuziba mwanya mpana uliopo kati ya kizazi cha jana na cha leo. Makala hii itaongozwa na nadharia ya uhalisia. Mhimili mkuu wa nadharia ya uhalisia ambao utaongoza makala ni kwamba, fasihi ni kioo cha jamii na inapaswa kumulika maisha kama yalivyo. Muundo wa kimaelezo utatumika kuchanganua data. Data itakusanywa kutokana na kusoma riwaya teule na kudondoa sehemu zinazolingana na malengo ya utafiti. Data itadondolewa, itanukuliwa, itapangwa kisha kuchanganuliwa kulingana na mada husika.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Vipengele vya Fasihi Simulizi Vinavyooana na Hali Katika Taaluma ya Sheria
    (East African Journal of Swahili Studies, 2020-06-10) Wekesa, Winnie Musailo; Simiyu, Fred Wanjala; Opande, Nilson Isaac
    Utafiti ulilenga kubainisha vipengele maalum vya Fasihi Simulizi vinavyooana na hali katika taaluma ya Sheria. Utafiti uliegemea uendeshaji wa kesi kitamaduni miongoni mwa jamii ya Babukusu. Ili kuafikia lengo hili utafiti ulitumia mbinu ya kithamano ya utafiti. Idadi lengwa ya utafiti ilikuwa jumla ya kesi za kitamaduni tulizohudhuria na kuzirekodi. Utafiti ulijumuisha michakato miwili ya uteuzi wa sampuli; ikiwa ni uteuzi sampuli kimaksudi na kinasibu. Uteuzi wa sampuli kimaksudi ulitumiwa kuchagua Chifu, naibu wa Chifu, mwenyekiti wa baraza la wazee na makala maalum yaliyoandikwa kuhusu Fasihi Simulizi na Sheria. Nao uteuzi wa sampuli kinasibu ulitumiwa kuteua mabaraza ya wazee na ya Chifu tulioyahudhuria. Waaidha, uchunguzi ulihusisha mbinu za uchambuzi wa yaliyomo, usaili na uchunzaji-shiriki. Njia hizi zilitumika kukusanya data nyanjani na maktabani. Matokeo ya utafiti yalichanganuliwa kithamano. Hii ni mbinu ya kuchanganua data ambayo mtafiti anaeleza na kufafanua matokeo ya utafiti wake kimaelezo. Kwa mujibu wa kesi tulizohudhuria, utafiti ulibaini kuwa kuna vipengele vya Fasihi Simulizi ambavyo vinaoana na hali ilivyo katika taaluma ya Sheria wakati wa uendeshaji kesi kitamaduni miongoni mwa jamii ya Babukusu. Kwa hivyo ni muhali kusema kuwa matini za Kifasihi Simulizi huwa zinachota, kunukuu, kugeuza, kuiga kwa namna ya kufumba, kubeza au kurejelea kwa njia moja ama nyingine matini za Kisheria. Hali kadhalika tanzu zenyewe za Fasihi Simulizi zinaingiliana na kuchangiana katika kutimiza mahitaji ya jamii kupitia shughuli mbalimbali.

DSpace software copyright © 2002-2026 LYRASIS

  • Privacy policy
  • End User Agreement
  • Send Feedback