Repository logo
Communities & Collections
All of DSpace
  • English
  • العربية
  • বাংলা
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Ελληνικά
  • Español
  • Suomi
  • Français
  • Gàidhlig
  • हिंदी
  • Magyar
  • Italiano
  • Қазақ
  • Latviešu
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Српски
  • Svenska
  • Türkçe
  • Yкраї́нська
  • Tiếng Việt
Log In
New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Ogola, James"

Filter results by typing the first few letters
Now showing 1 - 2 of 2
  • Results Per Page
  • Sort Options
  • No Thumbnail Available
    Item
    Itikadi za Ujinsia katika Maumbo ya Majina ya Kikuria
    (Ruwaza Afrika, 2023-03-11) Kasuma, Roseline; Ogola, James; Mohochi, Ernest Sangai
    Majina ni vipengele vya lugha ambavyo hutaja mtu, kitu, hali, mahali, dhana na tendo na huweza kufunua itikadi na matukio katika maisha ya wanajamii. Itikadi ni mawazo ambayo humwongoza kila mtu ulimwenguni katika kutenda anayotenda na hivyo kuhalalisha au kuharamisha matendo anayoyafanya. Makala haya yanajikita katika kuchanganua jinsi maumbo ya majina ya Kikuria katika jamii ya Wakuria iliyoko nchini Kenya hushamirisha itikadi za ujinsia. Itikadi za ujinsia ni imani, mielekeo na mitazamo inayoongoza jamii kuhusu mgawanyo wa majukumu kwa kuangalia jinsia. Lengo kuu la makala haya ni kuainisha jinsi maumbo ya majina ya Kikuria hudumisha na kuendeleza itikadi za ujinsia. Data iliyotumika katika makala haya ilikusanywa kwa njia ya mahojiano ya ana kwa ana na majadiliano ya makundi. Ukusanyaji na uchanganuzi wa data uliongozwa na Nadharia ya Onomastiki. Nadharia hii imekuwa dira katika kubainisha maumbo ya majina ya Wakuria na jinsi maumbo haya huakisi itikadi za ujinsia katika jamii ya Wakuria. Utafiti wetu uliweza kubainisha kuwa vipo vipashio ambavyo hudokeza jinsia na shughuli inayohusishwa nazo au nafasi yake katika jamii. Kwa misingi hii, utafiti wetu ulibainisha kuwa jinsia ya kiume kwa mujibu wa majina yao yaliyoteuliwa kiitikadi, ilitengewa shughuli na nafasi zilizoikweza ikilinganishwa na jinsia ya kike.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Mabadiliko ya Itikadi za Ujinaishaji katika Jamii ya Wakuria
    (Jarida la Kiswahili Sanifu, 2024-11-27) Mwikali, Roseline; Mohochi, Ernest Sangai; Ogola, James
    Dunia ya leo ya kiutandawazi inawezesha mtagusano wa umma wa kimataifa kidijitali unaoendelea kushuhudia utamaduni chipukizi wa ujinaishaji unaozidi kushika kasi. Hivyo, makala hii inachanganua mabadiliko katika ruwaza za ujinaishaji yanayotokana na athariya elimu ya magharibi, dini, teknolojia, na utawala katika jamii ya Wakuria pamoja na athari zake. Wakuria ni jamii ndogo ya kundi la Wabantu wa Magharibi inayopatikana katika Kaunti ya Migori nchini Kenya kwenye ujirani na nchi ya Tanzania. Ujinaishaji ni sehemu muhimu ya maisha ya jamii ya Wakuria kwani ni utambulisho wao. Aidha, sawa na jamii nyingine zile, ujinaishaji huwa dafina ya historia yao. Nadharia ya Uchanganuzi Hakiki wa Usemi mtazamo wa Kihistoria yao Wodak na Reisgil(2001)ilikuwadira katika uchanganuzi wa data zilizokusanywa. Data ambayo imetumika katika makala hii ilikusanywa kwa njia ya mahojiano ya ana kwa ana pamoja na majadiliano ya makundi. Idadi ya sampuli ilikuwa watu 42; wa kike 18 na wa kiume 24. Makala hii imebainisha kuwa mabadiliko ya kielimu, kiuchumi, kiteknolojia, kiutawala na kidini yamekuwa na athari kubwa kiitikadi katika ujinaishaji miongoni mwa Wakuria. Majilio ya elimu ya magharibi, uhuru wa kufanya biashara, mifumo ya kisiasa na mtagusano wa kiteknolojia umepelekea ukopaji wa majina kutoka makabila mengine nchini Kenya na ulimwenguni kote miongoni mwa jamii ya Wakuria. Hili linamaanisha kuwa itikadi za ujinsia zilizohodhiwa na kushamirishwa na majina ya kiasili ya Wakuria zinazidi kufifia kila uchao.

DSpace software copyright © 2002-2026 LYRASIS

  • Privacy policy
  • End User Agreement
  • Send Feedback