Repository logo
Communities & Collections
All of DSpace
  • English
  • العربية
  • বাংলা
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Ελληνικά
  • Español
  • Suomi
  • Français
  • Gàidhlig
  • हिंदी
  • Magyar
  • Italiano
  • Қазақ
  • Latviešu
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Српски
  • Svenska
  • Türkçe
  • Yкраї́нська
  • Tiếng Việt
Log In
New user? Click here to register. Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Wafula, Richard Makhanu"

Filter results by typing the first few letters
Now showing 1 - 2 of 2
  • Results Per Page
  • Sort Options
  • No Thumbnail Available
    Item
    Mapokeo ya Utenzi wa Mwana Kupona katika Upya wa Shaaban Robert: ‘Utenzi wa Hati’ na ‘Utenzi wa Adili’
    (East African Journal of Swahili Studies, 2024-07-11) Kinara, Gladys; Ngugi, Pamela Muhadia Yalwala; Wafula, Richard Makhanu
    Makala hii inalenga kuchunguza mapokeo ya Utenzi wa Mwana Kupona katika upya wa tenzi za Shaaban Robert: ‘Utenzi wa Hati’ na ‘Utenzi waAdili’ Robert (1967). Mapokeo yanaweza kuelezwa kama mila, desturi, fikra na hisia za kihistoria zinazohusu mtazamo sio tu wa yaliyopita zamani lakini pia uwepo wa mambo ya kihistoria na ya sasa kwa lengo la kuyapitisha kwa jamii (Sangi na wengine, 2012). Uchambuzi wa kazi hii umeegemezwa katika mihimili ya nadharia ya Bakhtin (1981) inayoshikilia kwamba lugha huwa na nguvu za Kani Kitovu na Kani Pewa. Kiwango cha Kani Kitovu huhusu nguvu za kisheria zinazotambulisha lugha. Hizi ni sheria za kisarufi na hazibadiliki. Katika muktadha wa fasihi, nguvu hizi zinawakilisha utamaduni wa jamii ambao daima unabaki kurithishwa na kufuatwa kama kanuni. Kiwango cha Kani Pewa nacho kinatokana na matumizi ya lugha katika jamii yanayobadilika kiwakati na yanatofautisha taaluma, tabaka na matumizi mengine ya lugha katika jamii. Nguvu za Kani Pewa zinajaribu kusukuma vipengele vya lugha kutoka katikati na kupelekea kuwa na wingi. Katika kiwango cha fasihi, nguvu za Kani Kitovu zinawakilisha utamaduni wa jamii ambao daima unabaki kurithishwa na kufuatwa kama kanuni. Kwa upande mwingine, kiwango cha Kani Pewa kinatokana na matumizi ya lugha katika jamii yanayobadilika kiwakati na yanayotofautisha taaluma, tabaka na matumizi mengine ya lugha katika jamii. Nguvu za Kani Pewa zinajaribu kusukuma vipengele vya lugha kutoka katikati na kupelekea kuwa na wingi. Katika kiwango cha fasihi, nguvu za Kani Pewa zinawakilisha upya na katika muktadha huu Utenzi wa Mwana Kupona katika tenzi za Shaaban Robert: ‘Utenzi wa Hati’ na ‘Utenzi wa Adili’. Utafiti ulikuwa wa kimaelezo na ulifanywa maktabani na nyanjani. Sampuli ya maktabani na nyanjani iliteuliwa kimakusudi. Maktabani, mtafiti alisoma kwa kina matini iliyochapishwa kwa lengo la kupata data ya msingi. Nyanjani, mtafiti alifanya mahojiano na majadiliano na wanajamii walioteuliwa katika kukusanya data. Data kutoka katika tenzi zilizoteuliwa, maandishi yaliyohusu utafiti, data ya nyanjani zilichambuliwa kulingana na lengo la makala haya na mihimili ya nadharia kwa lengo la kuonyesha namna mapokeo ya Utenzi wa Mwana Kupona yalivyobainika katika upya wa maandishi ya tenzi za Shaaban Robert: ‘Utenzi wa Hati’ na’ Utenzi wa Adili’. Matokeo ya utafiti huu yalibainisha kwamba Shaaban Robert (1967) katika kuandika ‘Utenzi wa Hati’ na’ Utenzi wa Adili’ aliazima pakubwa kutoka katika Utenzi wa Mwana Kupona mbali na kuongeza upya kwa mujibu wa hali ya kijamii ya wakati wake.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Upya wa Utenzi wa Mwana Kupona katika utenzi wa Howani Mwana Howani na Jawabu la Mwana Kupona
    (East African Journal of Swahili Studies, 2024-07-29) Kinara, Gladys; Wafula, Richard Makhanu; Ngugi, Pamela Muhadia Y.
    Makala hii ililenga kuchunguza upya wa Utenzi wa Mwana Kupona katika utenzi wa Howani Mwana Howani na Jawabu la Mwana Kupona. Makala hii iliongozwa na nadharia ya Bakhtin kuhusu lugha (1981) na Ufeministi wa Kiafrika iliyoasisiwa na Chioma (1980). Nadharia ya Bakhtin kuhusu lugha inashikilia kuwa lugha huwa na kani za aina mbili: nguvu za Kani Kitovu na Kani Pewa. Nguvu za Kani Kitovu zinafanya kazi kwa kuvuta vipengele vyote vya lugha na mbinu zake za ufasaha kuelekea katikati ili kutoa lugha moja iliyo sanifu au rasmi ambayo kila mmoja anaitumia. Nguvu hizo za Kani Kitovu zilikuwa kanuni zilozounganisha na kuleta kitu katikati. Nguvu za Kani Pewa zilijaribu kusukuma vipengele vya lugha kutoka katikati na kupelekea kuwa na wingi wa lugha au vijilugha. Kwa upande mwingine, Nadharia ya Ufeministi wa Kiafrika iliasisiwa katika miaka ya 1980 na Chioma na Kuendelezwa na Ogundipe (1994), Nnaemeka (2003) miongoni mwa wengine. Nadharia ya Ufeministi wa Kiafrika inafafanuliwa kama mapambano dhidi ya aina zote za dhuluma ili kupiga hatua katika kupata haki za wanawake. Jitihada hizi zinaweza kuwa za kijinsia, ubaguzi wa rangi, unyanyasaji wa kiuchumi kati ya dhuluma nyinginezo zinazolenga kumdhalilisha mwanamke (Bayu, 2019). Utafiti ulikuwa wa kimaelezo. Utafiti ulifanywa maktabani na nyanjani. Sampuli maktabani na nyajani iliteuliwa kimaksudi. Maktabani, mtafiti alisoma kwa kina matini iliyochapishwa kwa lengo la kupata data ya msingi. Nyanjani, mtafiti alifanya mahojiano na majadiliano na wanajamii walioteuliwa katika kukusanya data. Data kutoka katika tenzi zilizoteuliwa, maandishi yaliyohusu utafiti huu, data ya nyanjani zilichambuliwa kulingana na lengo la makala haya na mihimili ya nadharia kwa lengo la kuonyesha namna upya wa Mwana Kupona ulivyobainika katika utenzi wa Howani Mwana Howani na Jawabu la Mwana Kupona. Makala haya yalibainisha kuwa utenzi wa Howani Mwana Howani na Jawabu la Mwana Kupona zilisheheni upya kifani na kimaudhui katika mpito wa wakati.

DSpace software copyright © 2002-2026 LYRASIS

  • Privacy policy
  • End User Agreement
  • Send Feedback