dc.contributor.author | Magambo, Emilly Angushi | |
dc.contributor.author | Simiyu, Fred Wanjala | |
dc.contributor.author | Amukowa, Deborah | |
dc.date.accessioned | 2019-11-19T09:31:06Z | |
dc.date.available | 2019-11-19T09:31:06Z | |
dc.date.issued | 2019-08-23 | |
dc.identifier.uri | http://erepository.kibu.ac.ke/handle/123456789/1853 | |
dc.description.abstract | Utafiti huu ulichunguza mchango wa tamasha za muziki katika ufundishaji na
uainishaji wa nyimbo katika shule za upili nchini Kenya. Utafiti huu hasa
ulilenga kupambanua uainishaji wa nyimbo katika tamasha za muziki,
kudhihirisha namna uainishaji huu unavyoweza kutumiwa kufundishia
uainishaji wa nyimbo darasani na kuonesha namna ambavyo uainishaji wa
nyimbo katika tamasha za muziki huzisaidia nyimbo husika kutekeleza wajibu
wake. Tafiti nyingi zimefanywa kuhusu ufundishaji wa fasihi simulizi lakini
kuna haja ya kuchunguza njia mbadala za ufundishaji wa kipera cha nyimbo
kwa sababu ni kipana mno na hata uainishaji wake unakanganya. Utafiti huu
uliongozwa na nadharia ya utanzu inayoonesha utaratibu wa kuainisha fasihi
katika misingi ya aina mbalimbali kwa kuegemea miundo na maumbo, pamoja
na nadharia ya ujifunzaji kijamii ambayo inashikilia kuwa ujifunzaji ni
mchakato wa utambuzi ambao hujitokeza katika muktadha wa kijamii. Sampuli
iliyolengwa katika utafiti huu ilijumuisha shule zilizoshiriki katika mashindano
ya tamasha za muziki ya Kanda la Magharibi. Utafiti huu ulifanywa kwenye
mashindano ya tamasha za muziki kiwango cha kikanda eneo la Magharibi
yaliyofanyika katika shule ya upili ya wavulana ya Chavakali iliyo katika Kaunti
ya Vihiga nchini Kenya. Kauli mbiu yake ilikuwa kuboresha umoja wa kitaifa
kwa kuunganisha na kuleta watu pamoja. Watafitiwa ishirini na tano
walihojiwa. Mbinu ya kuteua sampuli ilikuwa ya kinasibu na ya kimakusudi.
Mtafiti alitumia utazamaji na mahojiano kama mbinu za kukusanya data.
Uchanganuzi wa data ulifanywa kwa kutumia maelezo ya kiufafanuzi na
kuwasilishwa kwa maandishi yaliyoambatana na mifano na picha. Mtafiti
alipata kwamba nyimbo zimeainishwa katika madaraja mbalimbali kutegemea
vigezo kama vile umri, mahali na maudhui. Utafiti huu ulibaini kuwa, tamasha
za muziki zinaweza kuwa njia mbadala ya kufundishia uainishaji wa kipera cha
nyimbo katika fasihi simulizi darasani. Umuhimu wa utafiti huu ni kuwa
matokeo yake yataweza kuwafaidi wana | en_US |
dc.language.iso | Swahili | en_US |
dc.publisher | Eanso | en_US |
dc.rights | Attribution-NonCommercial-ShareAlike 3.0 United States | * |
dc.rights.uri | http://creativecommons.org/licenses/by-nc-sa/3.0/us/ | * |
dc.subject | Masimulizi | en_US |
dc.subject | Mchakato | en_US |
dc.subject | Msuko | en_US |
dc.subject | Matukio | en_US |
dc.subject | Wahusika | en_US |
dc.subject | Maudhui | en_US |
dc.title | Mchango wa tamasha za muziki katika ufundishaji wa uainishaji wa nyimbo katika shule za upili nchini kenya | en_US |
dc.type | Article | en_US |